Loading...

Amana (Transactions)

Mwanachama anaweza kuweka fedha zake katika akaunti hii kiasi chochote anachoweza kwa hali ya usalama na kuzichukua wakati wowote anapohitaji.

  • Mwanachama anaweza kuweka Amana ya Muda Maalum na kupata faida kwa riba asilimia 7-9 kwa mwaka.
  • Mwanachama anaweza kumfungulia mtoto wake account ya amana toto
  • Mwanachama anaweza kutoa Amana zake Muda wowote
  • Mwanachama ataweza kupata Account statement

Mikopo (Loans)

Chama kinatoa mikopo ya elimu, biashara, kilimo na ufugaji, ujenzi, ununuzi wa vyombo vya usafiri, viwanja na shughuli zote za maendeleo. Muda wa marejesho ni mwezi mmoja (1) mpaka miezi 60 kwa riba nafuu sana. Kiwango cha juu cha mkopo ni TZS 40,000,000 kwa Mwanachama mmoja

  • Riba nafuu sana
  • Muda wa kutosha kwa urejeshaji
  • Mkopo kushughulikiwa ndani ya mda mfupi
  • kuanzia Tsh 50,000 hadi Tsh 40,000,000
  • Hakuna gharama kuomba mkopo

Hisa (Shares)

Mwanachama atanunua Hisa za msingi zisizopungua 70 sawa na TZS 700,000. (Thamani ya Hisa moja ni TZS 10,000) ili kumuwezesha Mwanachama kuwa mmiliki wa Chama. Mwanachama anaruhusiwa kununua Hisa za hiari (Zaidi ya TZS 700,000) ilimradi asizidi 20% ya Hisa zote za Chama.

  • Gawio kwa Mwaka
  • Kuwa na haki ya Kuchagua au kuchaguliwa kua Kiongozi
  • Kupata Cheti cha Umiliki
  • Kuhudhuria Mkutano Mkuu
  • Kuwa mmiliki kamili wa Chama

Akiba(Savings)

Mwanachama ataweka Akiba kwenye Chama kuanzia TZS 25,000 kila mwezi kulingana na uwezo na mipango ya Mwanachama. Akiba hii itakuwa dhamana ya mkopo na Mwanachama atakopeshwa mara nne ya Akiba zake na kwa kupata faida ya asilimia 7-9 kwa mwaka. Akiba haitachukuliwa na Mwanachama mpaka uanachama unapokoma.
Mwanachama ataweka Akiba ya dharura kwenye Chama kiwango cha juu TZS 600,000. Akiba hii itakuwa dhamana ya mkopo wa dharura na atakopeshwa mkopo wa dharura mara 5 ya Akiba ya dharura.

  • Akiba ni kigezo cha kupata Mkopo
  • Mwanachama ataweza kujua Salio la Akiba yake
  • Akiba ni Mustakabali wa Kesho yako
  • Mwanachama ataweza kupata faida ya asilimia 7-9 kwa mwaka

Kwanini Uchague Hai Rural Teachers SACCOS?

Tujali Wanachama

Bidhaa zetu zinakidhi Mahitaji ya Wanachama wetu wote.

Riba Nafuu

Furahia Mikopo ya Riba Nafuu kutoka Hai Rural Teachers SACCOS Ltd.

Usalama wa Fedha Zako

Fedha zako ziko salama na zimehakikishiwa kwa ulinzi wa juu ili kukupa utulivu na amani ya moyo

Msaada kwa Jamii

Hai Rural Teachers SACCOS Ltd husaidia katika kutatua changamoto, kuboresha maisha, na kukuza ustawi wa jamii kwa ujumla.

Uko Tayari Kuhakikisha Mustakabali Wako wa Kifedha?

Jiunge na maelfu ya Wanachama wa HRT SACCOS Ltd ambao tayari wananufaika na kuwa na maisha bora kupitia bidhaa zetu ikiwemo mikopo ya Maendeleo, mikopo ya dharura, Mikopo ya salary advance, Kuweka akiba, kuweka amana ya muda Maalum